Featured post

Jinsi ya kujitambulisha kwa Kiswahili(how to introduce yourself in Swahili)


Karibu kwenye makala yetu mpya! Leo, tutajifunza jinsi ya kujitambulisha kwa lugha ya Kiswaili. Iwe unasafiri kwenda Afrika Mashariki, unafanya biashara na wazungumzaji wa lugha ya kiswahili, au una nia tu ya kujifunza lugha hii nzuri, kujua jinsi ya kujitambulisha kwa usahihi ni hatua muhimu ya kwanza. Katika makala hihi tutakuongoja hatua kwa hatua kupitia misemo muhimu na mazungunzo rahisi ili uweze kujiamini unapokutana na watu wapya wanaozungumza lugha ya Kiswahili.

Welcome to our new article! Today we will look at how to introduce yourself in the Swahili language. Whether you are traveling to East Africa, doing business with Swahili speakers, or are simply interested in learning this beautiful language, knowing how to introduce yourself correctly is an important step. In this article we will guide you step-by-step through important phrases and simple conversation so that you can feel confident when you meet new Swahili-speaking people. Keep reading to learn!

Dialogue

George anajitambulisha kwa Zakaria(George introduces himself to Zakaria)

George: Shikamoo mzee!

Zakaria: Marahaba, hujambo?

George: Sijambo, mimi ninaitwa George. Na wewe unaitwa nani?

Zakaria: Mimi ninaitwa Zakaria. Wewe ni raia wa nchi gani?

George: mimi ni mmarekani. Ninatoka marekani, jimbo la Michigani.

Zakaria: Karibu sana Tanzania.

George: Asante sana. Wewe ni mtanzania?

Zakaria: Ndiyo! Mimi ni mtanzania. Ninatoka Arusha.

George: Asante sana, nimefurahi kukutana na wewe!

Zakaria: Nimefurahi pia. Kwaheri na karibu tena.

MSAMIATI(VOCABULARY)

Kiswahili/Swahili                  English

Nomino                                   Nouns

Arusha                                      A city in the Northern Tanzania

jimbo(ma-)                               State(s)

Marekani                                  America

Michigan                                  A state in the United states of America.

Mmarekani(wa)                        American(s)



Mzee                                          Elder/old person

nchi                                            Country/nation

raia                                             Citizen

Vitenzi                                       Verbs

itwa                                             be called

toka                                             come from



Semi Expressions

Shikamoo(greeing)                  I give you respect

Marahaba(greeting)                 I accept your respect

Ndiyo                                       positive response(yes)

hujambo?(greeting)                 How are you?

Sijambo(greeting)                   I am fine/well

Karibu sana                             You are very welcomed

Nimefurahi                              I am happy

kukutana                                  to meet



Viulizi Interrogatives

Gani?          which/what?

Nani?          Who?



MAELEZO YA SARUFI (GRAMMAR NOTES)

(a) Viwakilishi nafsi.(personal pronouns prefixes)

Persons

Example in word


1st person (ni)

ni-na-toka

ninatoka

2nd person (u)

u-na-toka

unatoka

3rd person (a)

a-na-toka

ninatoka



(b) Vivumishi vimilikishi(posessive adjectives)

Persons

Pronoun

Posessive adjectve

example


1st person

mimi

-angu

Jina langu

mine

2nd person

wewe

-ako

Jina lako

yours

3rd person

yeye

-ake

Jina lake

his/hers



(c) Kitenzi kuwa katika njeo ya wakati uliopo. (the verb to be (is/am/are) in the present tense.

ni(positive)                      si(negative)

mimi ni mtanzania          mimi si mtanzania

wewe ni mtanzania         wewe si mtanzania

yeye ni mtanzania           yeye si mtanziania.



(d) Utaifa (Nationality)

The prefix M-is attached to the name of the country to form nationality

Examples

Country          Nationality

Tanzania          Mtanzania

Ujerumani       Mjerumani

marekani         Mmarekani



Hivi ndivyo unavyoweza kujitambulisha kwa Kiswahili! Tunatumai umefurahia kujifunza misingi hii muhimu ya mawasiliano kwa kiswahili. Endelea kufanya mazoezi, na hivi karibuni utakuwa unazungumza kwa ujasiri zaidi. Asante kwa kusoma.

So, that is how you can introuce yourself in Swahili! We hope you enjoyed learning these basics of communication in Swahili. Keep practicing and soon you will be speaking with more confidence. Thank you for reading.

Comments

Popular posts from this blog

How to Greet in Swahili